Osama Al-Azhari ashiriki katika sherehe za siku ya kuzaliwa ya Mtume Mohammed (S.A.W) nchini India
Nemaa Ibrahim

Dkt. Osama Al-Azhari, Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Mambo ya Kidini na mmoja wa wanazuoni wa Al-Azhar Al-Sharif, anashiriki katika maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Mtume Mohammed (S.A.W) kwa kutoa mihadhara kadhaa huko India Kusini.
Al-Azhari alitembelea Chuo Kikuu cha Kituo cha Utamaduni cha Sunni huko Calicut, na vyuo vyake, taasisi kama vile Mji wa Maarifa na Msikiti wa Al-Futuh, kwa ufadhili wa msomi Sheikh Abu Bakr Ahmed, Mufti wa India na Katibu Mkuu wa Chama cha Wanazuoni wa Ahlus-Sunnah wal-Jama’ah nchini India yote, na kwa ufadhili wa mtoto wake mheshimiwa, Sheikh Dkt. Abdul Hakim bin Sheikh Abu Bakr, Mwenyezi Mungu awalinde.
Al-Azhari pia alitembelea Chuo Kikuu cha Utamaduni wa Ma’din katika mji wa Malabrom na vyuo na taasisi zake, chini ya ufadhili wa msomi Sheikh Ibrahim Al-Khalil Al-Bukhari, pamoja na kutembelea maktaba, taasisi za kitaaluma, nyumba za wasomi na watu wenye haki, shule zao na misikiti.