Habari Tofauti

Timu ya kitaifa ya utekelezaji wa  mradi wa  kuboresha elimu ya awali na Msingi wakutana

0:00

Timu ya kitaifa ya utekelezaji wa  mradi wa  kuboresha elimu ya awali na Msingi (Boost ) wamekutana  leo Julai 7, 2023 mkoani Morogoro katika kikao  kazi cha kuandaa taarifa ya utekelezaji wa mradi kwa  mwaka 2022/23 na  mkakati  wa utekelezaji wa  mradi kwa mwaka 2023/24.

Timu  hiyo inahusisha wataalamu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Taasidi ya elimu Tanzania , Wakala wa Maendeleo na Uongozi wa Elimu( ADEM) , Baraza la Mitihani na Tume ya Utumishi wa walimu (TSG).

Akitoa salamu kwa timu hiyo Katibu wa Tume ya Utumishi wa walimu Mwl.Paulina Nkwama kuhakikisha wanajadili kwa kina mpango kazi wa mradi  huo na kuhakikisha unaleta mabadiliko katika sekta ya Elimu

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa  ajili ya Sekta ya Elimu nchini hivyo amewataka wataalam kusimamia miradi ili iweze kukamilika kwa wakati

Back to top button