Habari Tofauti

Kozi ya 56 ya Waandishi wa Habari wa Afrika yazinduliwa

Mervet Sakr

Kozi ya 56 ya mafunzo kwa waandishi wa habari vijana wa Afrika, iliyoandaliwa na Muungano wa Waandishi wa Afrika inayoongozwa na Mahfouz Al-Ansari kwa kushirikiana na Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari linaloongozwa na Karam Gabr, ilianza Jumamosi mnamo Mei 6.

Wawakilishi wa nchi 15 za Afrika, pamoja na wawakilishi kadhaa wa magazeti ya kitaifa na ya chama, watashiriki katika kikao hicho.

Balozi Ahmed Hajjaj, Mshauri wa Muungano, alisema wakati wa ufunguzi wa kikao leo, “Tutasherehekea pamoja wakati wa kikao hiki Siku ya Afrika. Tutajadili jukumu la uandishi wa habari katika ngazi ya Afrika, wakati Dunia ikiadhimisha Siku ya Waandishi wa Habari Duniani mnamo Mei 3.”

Mwandishi wa habari Saleh Al-Salhi, Naibu Katibu wa Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari, alisema, “Itakuwa kozi katika ngazi ya kitaaluma, kubadilishana uzoefu, kujifunza kuhusu utamaduni wa Misri, kujadili masuala ya Afrika na mazingira yake, na dhamira yetu ni kulinda bara la Afrika na umoja wa nchi zake, ambayo ni jambo muhimu zaidi, na lazima ujenge uelewa miongoni mwa watu wa Afrika, kwani bara letu ni nyumbani mwetu sote, uandishi wa habari ni taaluma ya shida, uhuru wa vyombo vya habari ni wasiwasi wetu mkubwa, na uhuru wa maoni na kujieleza unahakikishiwa nchini Misri.”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Muungano wa Waandishi wa Afrika, Dkt. Samia Abbas, alithibitisha kuwa Muungano huo upo katika mchakato wa kuanzisha maktaba itakayojumuisha nyaraka na vitabu vyote vya masuala ya Afrika, ambavyo vitakuwa na mchango mkubwa katika kuwasaidia waandishi wa habari na wale wenye nia ya masuala ya Afrika kutekeleza wajibu wao.

Kikao hicho kimepangwa kujadili mada kadhaa, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Biashara Huria wa Afrika, uwezeshaji wa wanawake na vijana, uhusiano wa Misri na Afrika, jukumu la vyombo vya habari katika kujenga ufahamu wa watu, pamoja na mustakabali wa uandishi wa habari wa elektroniki, nishati katika Afrika, masuala ya mazingira na athari za operesheni ya kijeshi ya Urusi na Ukraine huko Afrika.

Kozi hiyo pia inajumuisha ziara za kikazi katika taasisi kadhaa za vyombo vya habari na miradi ya kitaifa ili kuona mafanikio Misri inayoshuhudia katika miundombinu katika ngazi zote, pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali ya utalii na akiolojia.

Back to top button