Habari Tofauti

Misri yatuma salamu za rambirambi kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa wahanga wa mafuriko mashariki mwa nchi hiyo

Mervet Sakr

 

Balozi Ahmed Abou Zeid, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, ametoa salamu za rambirambi za dhati za Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa wahanga wa mafuriko kutokana na mvua kubwa katika vijiji viwili katika mkoa wa mashariki wa Kivu Kusini, uliosababisha mamia ya waathirika, majeruhi na watu wasiojulikana.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wahanga na kuwatakia uchunguzi wa haraka watu waliopotea na kupona haraka kwa majeruhi, akisisitiza mshikamano wa Misri na serikali na watu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika msiba huo wa kusikitisha.

Back to top button