Habari Tofauti

Wizara ya Mambo ya Nje yaandaa Ziara ya Kikazi ya Mabalozi wa Marekani Kuelekea Aswan

Mervet Sakr

Balozi Dkt. Hazem Fahmy, Katibu Msaidizi wa Mambo ya Nje wa Masuala ya Marekani, akiwa ameambatana na mabalozi wa nchi za Marekani, alifanya ziara ya kikazi Kuelekea Aswan mnamo Aprili 11 na 12, ambapo ziara hiyo ilianza kwa mkutano na Meja Jenerali Ashraf Attia, Gavana wa Aswan, ambapo alikagua miradi ya mpango wa Rais “Maisha Bora”, pamoja na miradi ya “Aswan Mpya” na maendeleo ya barabara na miundombinu ndani ya Mkoa, ndani ya mfumo wa mpango wa serikali wa kujenga Jamhuri mpya.


Waziri huyo Msaidizi wa Mambo ya Nje, akiambatana na mabalozi wa nchi za Amerika walitembelea mtambo wa kuzalisha umeme wa jua wa “Benban” na uwekezaji wa dola bilioni 2, ambayo ni moja ya mitambo mikubwa zaidi ya nishati safi Duniani, na kushinda Tuzo ya Benki ya Dunia kama mradi bora zaidi wa nishati safi Duniani kwa mwaka 2018, pamoja na kiwanda cha mbolea cha “Kima 2”, ambacho Rais wa Jamhuri alikizindua mwaka 2021 na uwekezaji wa takriban dola milioni 800, na kwa teknolojia ya gesi asilia badala ya umeme wa maji kuzalisha urea na amonia, inayochangia Katika kukidhi mahitaji ya soko la ndani pamoja na soko la kimataifa kwa kuzingatia uhaba wa uzalishaji kutokana na mvutano uliopo kimataifa.

Ziara hiyo pia ilijumuisha Kituo cha Dkt. Magdy Yacoub cha Magonjwa na Tafiti za Moyo, kinachochukua nafasi ya kipekee Duniani katika kufanya shughuli nyeti za moyo kwa kutumia teknolojia za kisasa za kimataifa, zinazochangia kuokoa maisha ya maelfu ya wagonjwa kila mwaka.

Back to top button