
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaji DkT.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mama Mariam Mwinyi amefutari pamoja na Yatima, Walimu wa Madrasa ,Masheikh , Wajane ,Walemavu na Wazee wa Mkoa wa Kaskazini Pemba leo tarehe 12 Aprili 2023 ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba. .
Aidha, Rais Alhaji Dk.Mwinyi amehitimisha kufuturisha katika Mikoa ya Unguja na Pemba leo Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa makundi maalumu Mikoa yote .

Vilevile, DkT.Mwinyi amewahimiza waumini wa dini ya Kiislamu kuongeza jitihada kwa kufanya ibada katika kumi la Mwisho kwa Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.










