Habari

Balozi wa Misri ajadili njia za kuimarisha ushirikiano wa pande mbili na Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria

0:00

 

Balozi Mohamed Fouad, Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri nchini Nigeria, alikutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria, “Yusuf Tojar”, ambapo mkutano huo ulishughulikia njia za kuendeleza mahusiano ya nchi mbili kati ya Misri na Nigeria katika nyanja mbalimbali, haswa kuhusiana na kuimarisha ushirikiano katika uwanja wa biashara na uwekezaji, na maandalizi yanayoendelea kwa kikao cha tatu cha mashauriano ya kisiasa kati ya nchi hizo mbili katika robo ya mwisho ya mwaka huu, pamoja na mkutano wa Baraza la Biashara la Misri na Nigeria uliopangwa kufanyika Lagos mnamo Septemba 2024.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria aliomba kufikisha salamu za pongezi kwa Dkt. Badr Abdel Aty, Waziri wa Mambo ya Nje, Uhamiaji na Wamisri nje ya nchi, kwa tukio la kuchukua majukumu yake, akielezea nia yake ya kufanya kazi naye kuendeleza mahusiano ya nchi mbili kati ya nchi hizo mbili na kuimarisha uratibu uliopo kati yao katika masuala ya kipaumbele kwa Bara la Afrika.

Back to top button