
Jumanne,Rais Abdel Fattah El-Sisi amekutana mjini Sharm El-Sheikh na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Fakih.
Msemaji Rasmi wa Urais wa Jamhuri alisema kuwa mkutano huo ulijadili faili muhimu zaidi kwenye Ajenda ya Umoja wa Afrika, hasa kuhusiana na Ushirikiano wa kiuchumi na kikanda, Amani na Usalama, na mageuzi ya kitaasisi ya Muungano, ambapo ilikubaliwa kuendelea ushirikiano wa karibu na uratibu kati ya pande mbili katika suala hili, kwa kuzingatia Misri kuwa moja ya nguzo muhimu za kuendeleza hatua za pamoja za Afrika, na katika juhudi za kuongeza faida ya jukumu la kisiasa na maendeleo la Misri, ili kutumikia maslahi ya bara la Afrika kwa ufanisi.










