Habari

Rais El-Sisi azindua mikutano ya kila mwaka ya Benki ya Maendeleo ya Afrika

Mervet Sakr

Rais Abdel Fattah El-Sisi amefungua mikutano ya kila mwaka ya Benki ya Maendeleo ya Afrika, iliyoandaliwa na Misri huko Sharm El-Sheikh, kwa kauli mbiu ya “Kuhamasisha Fedha za Sekta Binafsi kwa ajili ya Hali ya Hewa na Ukuaji wa Kijani Barani Afrika”.

Mshauri Ahmed Fahmy, Msemaji Rasmi wa Urais wa Jamhuri, alisema kuwa ufunguzi huo ulishuhudia ushiriki wa wakuu kadhaa wa nchi na serikali ya nchi ndugu za Afrika, taasisi mbalimbali za kikanda, pamoja na idadi kubwa ya mawaziri wa fedha, magavana wa benki kuu, wawakilishi wa sekta binafsi, wasomi na washirika wa maendeleo kutoka nchi wanachama wa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Rais alitoa hotuba katika hafla hiyo, ambapo alielezea kufurahishwa kwa jukumu muhimu linalofanywa na Benki ya Maendeleo ya Afrika katika kusaidia masuala ya maendeleo Barani Afrika, haswa kutokana na changamoto za kiuchumi zinazoongezeka katika ngazi ya kimataifa.

Rais pia alisisitiza kuwa Misri inaendelea kuunga mkono juhudi za kufikia maendeleo ya kiuchumi kwa nchi za bara la Afrika, iwe katika ngazi za kikanda au kimataifa.

Back to top button