RAIS DKT.MWINYI AVITAKA VIKUNDI VYA MAZOEZI KUIBUA FURSA ZA MIRADI YA UJASIAMALI NA KUSAFISHA MAZINGIRA
Ahmed Hassan

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi awapongeza Chama cha Mchezo wa Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA), kwa utaratibu wa kuwaunganisha wananchi kwa kufanya Mazoezi kwa kuimarisha afya za watu , kuwaweka pamoja kwani umoja wao unaweza kuleta tija kwa maendeleo katika kuibua fursa mbalimbali kwa vikundi hivyo .
Rais Dkt.Mwinyi aliyasema hayo alipokutana na Uongozi wa Chama cha Mchezo wa Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA) , ukiongozwa na Mwenyekiti wake Said Suleiman Said.
Dkt.Mwinyi amesema hamasa inayotolewa katika ufanyajaji Mazoezi ni njia sahihi katika kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni hamasa yenye tija, pia amewaasa kuendelea kuwashawishi wananchi zaidi waendelee kujiunga katika vikundi hivyo walio katika vikundi wasitoke.
Rais Dkt.Mwinyi amewaunga mkono na kuwapongeza kwa utaratibu wa kufanya usafi katika kisiwa cha Changuu na ameunga mkono wazo la Siku ya Jumamosi kuwa siku ya usafi na ameshauri ili vikundi viwe kimaendeleo zaidi katika Uanzishwaji wa shughuli za uzalishaji mali kwa maana inakuwa rahisi kwa Serikali kuwasaidia wakiwa katika vikundi .
Dkt.Mwinyi amewataka ZABESA kushirikiana na sekta binafsi hasa makampuni ya simu na benki kufanikisha matamasha yao kufikisha ujumbe kwa jamii kuhusu ufanyajaji Mazoezi na usafi wa Mazingira .
Dkt.Mwinyi amewaahidi kushirikiana nao kutafuta waatalamu wa Mazoezi ambao watakuwa watajitolea kufundisha vikundi mbalimbali aina za ufanyaji wa Mazoezi.
Naye , Mwenyekiti wa chama hicho ndugu Said amempongeza Rais Dk.Mwinyi kwa kutimiza miaka miwili ya Uongozi wake kwa Maendeleo anayowaletea Wazanzibari , pia kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar.
Ndugu Said , amesema wataunga mkono juhudi za Serikali na kubuni miradi mbalimbali mbadala ya kuhifadhi takataka .
Alisema ZABESA imejipanga kuungana na Dunia kuadhimisha siku ya Usafi Duniani inayo adhimishwa kila Jumamosi ya tatu ya Mwezi wa Septemba kila Mwaka.
Vile vile, wamesema ZABESA ina lengo la kugeuza mtazamo wa kimazoezi na uwe Mazoezi kwa afya na maendeleo tofauti kwa sasa.