Watawala Wa Misri

Mohamed Hosni Mubarak

0:00

Muhammad Mubarak alizaliwa mnamo Mei 4, 1928, na alikulia katika familia ya hali ya wastani katika Mkoa wa  Menufia, na alisoma katika Kitivo cha Kijeshi na akahitimu kutoka kwake mnamo 1950 , na alichaguliwa kuwa afisa katika Jeshi la Anga,kisha alipata Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya Usafiri wa Anga ili aweze kufanya kazi hapo katika viwanja vya ndege vingi vya Misri.

 Alipewa kazi ya ufundishaji katika Kitivo cha Jeshi la Wanahewa kwa sababu ya kiwango chake cha juu cha masomo na uratibu wake, na alibaki katika kufundisha kutoka 1952 , kupitia matukio ya Mapinduzi ya Julai hadi 1959 , na aliwasomesha vikundi kadhaa vya wanafunzi.

Mubarak pia alipata masomo yake ya uzamili katika Chuo cha Sayansi cha Bronze mnamo 1964, na akapandishwa katika madaraka kadhaa hadi akaongoza ujumbe wa kijeshi wa Umoja wa Kisovieti.

Mnamo Novemba 1967, aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa Kitivo cha Jeshi la Anga, na cheo chake wakati huo kilikuwa Kanali. Mnamo Juni 1967, miezi kadhaa baada ya kumalizika kwa Vita, aliteuliwa na Rais Gamal Abdel Nasser kama Mkuu wa Wafanyakazi wa Anga.Na alimshikilia cheo cha Kiongozi mkuu kabla ya marafiki zake kwa siku kumi na hivyo kwa mujibu wa uhodari wake na uzoefu wake mzito wa kisayansi na wa vitendo.

Mwezi na siku kumi baadaye Mubark akashangaa kwani alipandishwa cheo kwa mara ya pili na Rais Abdel Nasser na akawa Jenerali, na mnamo Aprili 1972 Rais Al-Sadat akamshikilia  uongozi wa jeshi la Wanahewa, kwa hivyo Mubark alichangia vizuri sana kwa jukumu la kihistoria  ambapo watu wa Misri walipata tena heshima yao katika Vita  tukufu vya  Oktoba Sita.

Mnamo Aprili 1975,Mubark aliteuliwa kuwa makamu wa Rais Al-Sadat hata alipouawa, na wajumbe wa Bunge walimchagua Mubark kuwa Rais wa Jamhuri basi akachaguliwa tena kuwa Rais wa nchi katika maoni ya kiraia kwani ni mgombea pekee mnamo miaka kadhaa  1987,1993, na 1999 ambapo Katiba ya Kimisri ilichagua muda ya urais usiozidi miaka sita kuhusu mara ambazo anaweza kugombea.

Mnamo mwaka wa 2005,Mubarak alifanya marekebisho ya katiba yaliyofanya uchaguzi wa Rais ukawa kura ya siri ya moja kwa moja na uteuzi umefunguliwa na viongozi wa chama ,na alichaguliwa tena kwa kiwango kikubwa kutoka wapiga kura.

Pia alichangia sana  katika mazungumzo ya Amani yaliyoanzishwa na Rais Al-Sadat,na aliweza kurudisha Taba mwaka 198.
Na wakati wa enzi yake ulishuhudia miradi muhimu kadhaa kama Treni ya Metro huko Kairo na Giza,Mfereji wa Al-Salaam huko Sinai ,Mradi wa Toshka na Mashariki ya Al-Owainat.

Mubarak aliendelea kuwa Rais wa  Jamhuri ya Kiarabu ya Misri kwa takriban miaka 30 hadi mapinduzi ya Januari 25,2011 yakidai kuondoa utawala wake,na kweli Mubarak aliondoka madarakani Febuari 11 mwaka huo huo.

Mubarak aliaga Dunia mnamo Febuari 25,2020,na mazishi ya kijeshi yalifanyika kwake kwa mahudhurio ya Rais El-Sisi,mawaziri kadhaa na viongozi wa nchi.

Check Also
Close
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"