Watawala Wa Misri

Ibrahim Pasha

0:00

Mtawala wa Misri kutoka kipindi cha Septemba 2, mwaka 1848 hadi Novemba 10, mwaka 1848.

 Amechukua nafasi mbalimbali za usimamizi wa kiraia na kijeshi, kabla ya kuchukua utawala wa Misri. Amejali kilimo, kuanzisha benki ya mikopo ya kilimo, kujali biashara ya sukari, kuanzisha kiwanda cha kusafisha sukari. Amekuwa kupendeza uhuru wa biashara badala ya njia ya ulanguzi (kuhodhi bidhaa ) ambayo Mohamed Ali Pasha –baba yake- aliiweka.

Amezaliwa mnamo 1789, kijijini Nasratly, nchini Ugiriki.

Agosti 28, mwaka 1805, aliteulewa kama mtawala wa ngome wakati wa kufikia kwake nchini Misri pamoja na familia yake.

Desemba 13, mwaka 1807, alirudi Misri kutoka Istanbul, na kuchukua nafasi ya Waziri wa fedha (Daftardaria).

Aprili, mwaka 1812, alichukua utawala wa Misri ya juu, na kuujumuisha na nafasi ya Wizara ya fedha ( Daftardaria).

Mwaka 1813, alichukua nafasi ya afisa wa eneo la mpaka wa kimisri, na kwa maagizo ya Mohamed Ali Pasha, alihesabu ardhi za kilimo, kupanga daftari za eneo zilizokuwa mafanikio muhimu zaidi ya ujenzi ya Mohamed Ali Pasha.

Mohamed Ali alimfanya kuwa kiongozi wa jeshi la Misri katika vita vya Kiwahabi (1816-1819), na alifanya ushindi mkubwa.

Mwaka 1829, amekuwa kiongozi wa baraza la washauri, moja ya utaalamu wake ilikuwa kutafiti katika masuala ya usimamizi wa kiraia na kijeshi, na alifanya matengenezo makubwa katika kurugenzi la mashariki.

Sultani wa Othomani alimpa mkoa wa Jeddah na vifaa vyake, na usheikhe wa msikiti mkuu wa Makka na Madina.

Alipata usimamizi wa vikosi vya kimisri katika vita vya Ugiriki na vita vya Sham, alishinda katika vita mbalimbali, ameweza kuingia Dameski, na alishinda waturuki katika vita vya Konya.

Septemba 2, mwaka 1848, amri kutoka mlango wa juu ilitoewa kuhusu kupata kwake kwa utawala wa Misri, kwa sababu ya maradhi ya Mohamed Ali Pasha.

Amepa ardhi za kilimo kwa nani anayetaka kuzipanda, kuzisamehe kutoka kodi iwapo zinataka kukarabati, na kuanzisha benki ya mikopo ya kilimo kwa kutoa mikopo muhimu kwa kupanda ardhi.

Alijali biashara ya sukari, amepanda sukari katika maeneo makubwa; alianzisha kiwanda kilichofanywa kwa mvuke kwa kusafisha sukari, kama alianzisha kiwanda kilichojulikana na ikulu ya juu.

Aliingiza matengenezo katika mfumo wa korti ya kibiashara, amekuwa alipendeza uhuru wa biashara badala ya mfumo wa kuhodhi ambao Mohamed Ali Pasha aliuweka.

Idadi ya ngome imezidi kwa ngome ishirini na tano  wakati wa utawala wake, kujali kuendelea ngome za Aleskandaria, na kuizidi kwa askari na silaha, kama ameamua kuchimba njia ya kijeshi kutoka Aleskandaria kwa Abu Keir na Rashid kwa kupokeza askari na silaha kwenye ngome.

Aliweka mpango maalum kwa kuanzisha shule za serikali katika miji mikuu, kama mfumo unaofuatiwa nchini Misri.

Alikufa Novemba 10, mwaka 1848.

Check Also
Close
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"