Watawala Wa Misri

Sultani Hussein Kamel

0:00

Mtawala wa Misri mnamo kipindi cha (Desemba 19, 1914 – Oktoba 9, 1917).

Amechukua nafasi kadhaa za usimamizi kabla ya kushika Madaraka, alilinda nchi kutoka Janga la mafuriko ya Nile kwa kuchukua tahadhari zote ili kulinda na kuimarisha madaraja. Naye ni wa kwanza aliyeanzisha maonyesho ya kilimo nchini Misri, pia amekuwa mtawala mmisri wa kwanza  ambaye pesa zilichapishwa kwa jina lako.

 Amezaliwa Novemba 21, mwaka 1853, mkoani Kairo.

Amepata elimu yake shuleni Al Maneil, kisha alisafiri Ufaransa, mwaka 1868, ambapo alikaa katika korti ya Napoleon Bonaparte wa tatu.

Amerudi nchini Misri wakati wa ufunguzi wa mfereji wa Suez, na alikuwa mkalimani wa malkia Eugenie.

Khedevi Tawfik alimwuliza kukaribisha  mfalme Edward VII –mrithi wa utawala wa Uingereza-, na kaisari Nicholas II –mrithi wa utawala wa Urusi”.

Alipata nafasi ya mkaguzi mkuu wa mikao ya kibahari na juu ya Misri, mwaka 1872, kisha Wizara ya kazi za umma, kisha Wizara ya fedha, kisha utawala wa Jumuiya kuu, na baraza la Ushauri la Sheria.

Alipata utawala wa Misri baada ya azimio la ulinzi wa Uingereza mnamo Desemba 19, mwaka 1914.

Ameanzisha reli zilizoungana mkoa Helwan na mji mkuu.

Aliamua kutoa zawadi kwa wanafundhi hodari, lililosabibisha nguvu katika ushindani wa kisayansi kati ya wanafunzi, na kuboresha kiwango cha mchakato wa elimu, ameanzisha shule za kijeshi za watoto mkoani Kairo na Aleskandaria.

Mtawala mmisri wa kwanza ambaye pesa zilichapishwa kwa jina lako baada ya kumaliza  kwa utawala wa Ottoman.

Aliaga Dunia mnamo Oktoba 9, mwaka 1917.

Check Also
Close
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"