Misri moja ya nchi 10 zinazokua kiuchumi kwa kasi duniani mwaka 2022

Kituo cha Habari cha Baraza la Mawaziri kilichapisha video ya muhtasari wa matukio ya 2022 katika ngazi ya ndani nchini Misri.
Kituo hicho kilieleza kuwa mwaka wa 2022 ulishuhudia juhudi na maendeleo mengi, licha ya matatizo ya kimataifa ambayo dunia iliyapata katika mwaka huo ambayo yameweka kivuli katika uchumi mbalimbali, ikibainisha kuwa Misri ilivuta macho ya dunia katika uwezo wake wa kukabiliana na kuwekeza katika migogoro na ilikuwa. miongoni mwa nchi 8 zilizo bora zaidi barani Afrika katika orodha ya malengo ya maendeleo endelevu.
Video hiyo ilionesha kuwa Misri ni ya kwanza katika miradi ya hoteli barani Afrika 2022, na ya tano duniani katika faharasa ya matumizi ya nishati kulingana na Kielezo cha Utendaji Kazi cha Mabadiliko ya Tabianchi 2023, kuruka nafasi 42 katika faharasa ya kustawi kw serikali ya kidijitali kwa mwaka 2022, ili iwe miongoni mwa nchi 10 zinazokua kiuchumi duniani mwaka 2022, kulingana na Mfuko wa Fedha wa kimataifa.
Mfumo wa kwanza wa baiskeli ambao ni rafiki kwa mazingira pia ulizinduliwa nchini Misri, operesheni ya kwanza ya upandikizaji wa mapafu ilifanywa nchini Misri katika Hospitali ya Ain Shams, na “Safari ya Familia Takatifu” kwenda Misri ilisajiliwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia wa UNESCO.