Balozi wa Misri nchini Burundi atoa Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi

Mnamo Februari 15, Balozi Amira Abdel Rahim, Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri nchini Burundi, alikabidhi hati zake za utambulisho kama Balozi wa Jamhuri ya Burundi kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye.
Balozi Amira Abderrahim alibainisha mahusiano mazuri kati ya nchi hizo mbili na kuelezea nia yake ya kushirikiana na maafisa wa Burundi kutumikia maslahi ya pamoja. Pia alisisitiza hamu yake katika uratibu na ushirikiano wa kudumu kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa ya maslahi ya pamoja, na msaada wa pamoja kati ya nchi mbili ndani ya mfumo wa vikao vya kikanda na kimataifa.
Kwa upande wake, Rais wa Burundi ameelezea kufurahishwa kwake na mahusiano kati ya nchi hizo mbili, na pia alitoa salamu zake kwa nduguye, Rais Abdel Fattah El-Sisi na alionesha furaha yake kwa ziara yake ya awali nchini Misri, akiielezea kama nchi iliyobarikiwa, na kusisitiza nia yake ya kuendelea na mawasiliano na uratibu ili kukuza maslahi ya Misri na Burundi.










