Utambulisho Wa Kimisri

Dokta Ahmed Zewail

0:00

Ni mtaalam wa kemia na mwanasayansi mmisri

Aliyepewa Tuzo ya Nobel katika Kemia mnamo 1999 kwa kuunda mfumo wa kupiga picha wenye upesi mkubwa sana kupitia kutumia  laser unaoweza kugundua harakati za masi wakati zinatokea na zinapojumuika pamoja.  Na kiasi cha wakati kinachotumika kwa jambo hilo ni Femto sekunde  nacho ni  sehemu moja  toka dola milioni sehemu ya sekunde moja  , kimechangiakutambua magonjwa mengi haraka, pia ana vyeti  vingi vya kubuni vifaa vingi vya kisayansi.

Malezi na elimu yake

Ahmed Hassan Zewail alizaliwa mnamo 1946 huko Damanhour, alielekea pamoja na familia yake kwenye mji wa Desouk mkoa wa Kafr El Sheikh, ambapo aliishi na alipata elimu yake ya kimsingi.

Alijiunga na Kitivo cha Sayansi, Chuo Kikuu cha Aleskandaria  baada ya kupata shule ya sekondari na kupata Shahada ya Sayansi kwa cheti cha  heshima mnamo 1967 katika utaalam wa Kemia, na alifanya kazi kama mhadhiri katika kitivo , baadaye akapata cheti cha uzamili katika uwanja wa sayansi ya Mwangaza.

Alisafiri kwenda Marekani katika udhamini wa kimasomo  na akapata uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Pennsylvania  katika  taaluma za laser huko  Marekani.

Nafasi alizozipata:

– Alifanya kazi kama mtafiti katika Chuo Kikuu cha California (1974-1976) na kisha akahamia Chuo Kikuu cha Caltech,  nacho ni kimoja cha vyuo vikuu vikubwa vya sayansi huko Marekani.

– Alielekea katika nafasi za masomo ndani ya Chuo Kikuu cha “Caltech” hadi kuwa profesa wa uwanja wa Kemia, ambayo ndiyo nafasi ya juu zaidi ya kisayansi huko Marekani, akikuja kufuatia mwanasayansi wa Marekani “Linus Pauling,” aliyeipata tuzo ya Nobel mara mbili, ya kwanza katika Kemia na ya pili katika Amani.

– Alichapisha  tafiti zaidi ya 350 za kisayansi katika Magazeti maalum ya kisayansi ya kimataifa kama vile Gazeti la Science na Nature.

– Alifanya kazi kama profesa mgeni katika vyuo vikuu zaidi ya 10 ulimwenguni pamoja na Chuo Kikuu cha Marekani  huko Kairo.

–  Alitoa Mamia ya mihadhara ya kisayansi ulimwenguni kote, na jina lake lilitolewa katika orodha ya heshima huko Marekani , inayojumuisha wahusika muhimu zaidi waliochangia katika ustawi wa kimarekani, na alipewa jina Na 18 kati ya watu 29 mashuhuri kama wanasayansi muhimu wa laser huko Marekani  (orodha hii inajumuisha Einstein, Na Graham Bell).

Tuzo na Heshima

Dokta Ahmed Zewail amepokea sifa , tuzo, na nishani nyingi za kimataifa kwa utafiti wake wa upainia katika sayansi ya laser na femto, ambapo ameshinda tuzo za kimataifa 31, pamoja na:

  • Tuzo ya Max Planck, nayo ni ya kwanza nchini Ujerumani.
  • Tuzo ya “Walsh” ya kimarekani.
  •  Tuzo ya Harion How ya kimarekani .
  • Tuzo ya Kimataifa ya mfalme Faisal katika Sayansi.
  • Tuzo ya Hoekst ya Ujerumani .
  • Alichaguliwa kama mshiriki wa Chuo cha Sayansi na Sanaa cha Marekani.
  •  amepewa medali ya Chuo cha Sayansi na Sanaa ya Uholanzi.
  • Tuzo ya Ubora kwa jina la Leonardo da Vinci.
  • Alipata uzamivu wa  heshima kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, Chuo Kikuu cha Marekani huko Kairo na Chuo Kikuu cha Aleskandaria.
  • Tuzo ya Alexander von Humbolden kutoka Ujerumani Magharibi nayo ni  tuzo kubwa zaidi ya kisayansi huko.
  • Tuzo ya Buck na Tine kutoka New York.
  • Tuzo ya Mfalme Faisal katika Sayansi na Fizikia mnamo 1989.
  • Tuzo katika Kemia mnamo 1993.
  • Tuzo ya Benjamin Franklin mnamo 1998 kwa kazi yake katika utafiti wa athari za kemikali kwa wakati mdogo sana (Femto-Second) inayoitwa femtochemistry.
  • Tuzo ya Nobel kwa Kemia kwa mafanikio yake katika uwanja huo huo mnamo 1999.
  • Imechaguliwa na Chuo cha Pontifical, kuwa mshiriki na kupokea nishani yake ya kidhahabu mnamo 2000
  • Tuzo ya Wizara ya Nishati ya Marekani  ya kila mwaka katika Kemia.
  • Tuzo ya Kars kutoka Chuo Kikuu cha Zurich, katika kemia na Tabia,  nayo ni tuzo kubwa zaidi ya kisayansi ya Uswizi.
  • Alichaguliwa kwa hiari mwanachama wa Chuo cha Sayansi cha Marekani.
  • Jina lake liliwekwa kwenye orodha ya heshima huko Marekani.
  • Misri ilimheshima, ambapo alipokea tuzo kadhaa za kimisri, pamoja na nishani kuu ya daraja ya kwanza kutoka Rais Hosni Mubarak mnamo 1995, na Mkufu Mkuu wa Nile, nishani ya juu kabisa ya kimisri, na jina lake likaitwa katika mitaa na viwanja kadhaa, na Mamlaka ya Posta  ilitoa stampu mbili kwajina na sura yake, na jina lake lilitolewa kwa Sebule ya Opera.
  • Mnamo Aprili 2009, Nyumba nyeupe” White House” ilitangaza uteuzi wa Dokta Ahmed Zewail yuko kwenye Bodi ya Washauri ya Rais wa Marekani  ya Sayansi na Teknolojia, inayojumuisha wanasayansi 20 wanajulikana katika nyanja kadhaa.

Maandishi  yake

Dokta Ahmed Zewail alitunga vitabu viwili navyo ni :

– Kitabu cha safari kupitia wakati .. njia kuelekea Noble.

–  kitabu cha Enzi ya sayansi: Iliyotolewa mnamo 2005, na mnamo mwaka mmoja ilichapishwa matoleo 5, ambapo toleo  lake la kwanza  lilimalizika wakati  wa masaa mawili ya kuchapishwa kwake.

Kifo chake

Aliaga dunia  mnamo 2/8/2016 na alipendekeza azike huko Misri.

Check Also
Close
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"