Miji Ya Misri

Mji wa Suez..Ardhi ya Vita na Mapambano

0:00

Farau wa Miradi aliichukua kituo cha operesheni zake za kijeshi ili kulinda  migodi ya Sinai na kuwazuia wakoloni na aliipewa jina la SICOT mwaka wa 2563, na katika zamu ya nasaba ya 19 na 22 iliitwa (U – SWITES), kisha iliipewa jina la (Uswites), na wakati wa utawala wa Giriki iliipewa jina la (Heropolis) yaani mji wa mashujaa, na wakati wa utawala wa  Cleopatra aliita (Cleo Patress), na mnamo karne ya 19 Khamariwiya bin Ahmed bin Tolon waliita (Suez) na kiongozi marehemu Gamal Abdel Nasser aliisifu “Hamna nchi jina lake limehusishwa na historia kama Suez”.

Suez inachukuliwa kuwa njia ya Afrika na nchi  za kusini magharibi na mashariki ya Asia, jambo ambalo liliifanya kitou cha mkutano wa biashara ya kimataifa na njia ya urembazaji kati ya mashariki na magharibi na ngome ya viwanda na uwekezaji wa viwanda ambapo ilikuwa moja ya bandari muhimu zaidi ya mashariki ya kati kwa karne nyingi. Na mwonzoni ilijulikana kwa jina la Qalzum .Na jina hili limechapishwa katika bahari nyekundu yote. na hilo lilikuwa linajulikana kihistoria kama bahari ya ElQelzum.Hata jina lake lilipobadilisha kwa Suez ilickukua jina lake kutoka Ghuba hii kubwa  inayojumuisha pande ya pili ya bahari nyekundu Ghuba ya  Suez.

“Al Qulzum” au Suez Canal baadaye, ni bandari kuu kwa Misri  kwenye bahari  nyekundu, pia ilikuwa njia na kituo vya Wahaji na  wanaofanya Umrah wanaokuja kutoka nchi tofauti za Afrika wakielekea kisiwa cha Uarabuni, na  Kitu kinachoandaliwa huko Misri kila mwaka kwa ajili ya kufunika  Kaaba ,kilikuwa kinapitia kwenye bandari ya Khor na kwa miaka kumi na zaidi ilibaki Bandari muhimu zaidi baharini nyekundu.

Bendari ya Suez ilishuhudia mwanzo wa vita vya Muhammad Ali Pasha kwenye kisiwa cha Uarabuni na kabla ya kuchimba mfereji wa Suez , Misri tayari ilkuwa mojawapo ya njia muhimu zaidi kwa biashara ya kimataifa inayoitwa biashara ya Tranzeet, ambapo
Misri pamoja na eneo la kijiografia ambalo lilisaidia mashariki na Magharibi yakutane pamoja, ilikuwa ikikaribisha Biashara ya kimashariki zinakuja  kutoka Asia ili kusafirishwa kwenda Ulaya, na pia bidhaa za Ulaya  na silaha ili  kusafirishwa kwenda Asia, na njia kuu ya biashara hiyo  ilkuwa Alexandria – Cairo_ Suez na kinyume.

Wakati Ufaransa iliishauri Misri mradi wa Suez Canal mnamo katikati ya karne ya 19 ,Uingereza ilikataa mradi huu mwanzoni kwani iliona ni mwanzo kurudi ushawishi wa Ufaransa kwa Misri mara tena baada ya Uingereza ilifanikwa kufukuza kampeni ya Ufaransa kutoka Misri hivyo Uingereza ilitoa pendkezo kuanzisha mradi mwingine Kushinda  mradi wa Suez Canal ,nao ni kuimarisha njia ya nchi kavu ya kawaida  kwa biashara: Alexandria _ Cairo _ Suez kupitia kuanzisha njia ya reli, na labda hiyo ni sababu kuu ya kupatikana Reli nchini Misri kama moja ya nchi za kwanza kufahamu njia ya Reli.
Miongoni mwa sababu kuu za kusimamisha ukuaji wa Suez wakati huo ilikuwa uhaba wa maji safi, ambapo Maji yalisafirishwa kwenda kwake kwa ngamia, kutoka macho ya Musa, iliyoko kilomita 16 kusini mashariki mwa Suez, na Ofisi za makampuni ya usafirishaji na hoteli za kigeni huko Suez zilitegemea kubadilisha maji ya bahari kuwa maji safi ili kuwahudumia wafanyakazi na wageni wao, pia wakati reli ya Kairo-Suez ilipojengwa, serikali ya Misri ilisafirisha maji kutoka Kairo hadi Suez, katika meli za mafuta. Serikali ilikuwa inauza maji kwa wananchi.

Kwa hivyo, uchimbaji wa Mfereji Mtamu wa Suez ni moja ya mambo muhimu yaliyosababisha maendeleo ya mji na ukuaji wa miji ndani yake. Kweli, mradi wa kuchimba mfereji huu ulihusishwa kwa karibu na mradi wa mfereji wenyewe, na Kampuni ya Mfereji wa Suez hata ilifikiria kuwa uchimbaji wa mfereji huu unapaswa kuwa kabla ya kuchimba mfereji, ili kutodanganya shughuli za kuchimba visima, kama ilivyotokea mnamo miaka minne ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa kuchimba mfereji, katika nusu ya kaskazini ya Suez Isthmus, kati ya Port Said na Ziwa la Mamba.

Mfereji huu mpya ulijulikana kama “Mfereji wa Ismailia”, na mwanzilishi wa ufufuo wa miji ya kisasa ya Misri, na mwanahistoria na mtaalamu wa elimu wa Misri na ufufuo mkubwa wa elimu uliopewa jina la utani “Baba wa Elimu” Ali Mubarak anaonesha umuhimu wa Mfereji wa Ismailia, na athari zake kwa maendeleo ya mji wa Suez, katika “mipango ya Maelewano”, kwa kusema: “Moja ya sababu kubwa ya usanifu wa mji wa Suez, kuwasili kwa maji ya mto Nile kwake, kutoka mfereji wa Ismaili, ulioanzishwa wakati wa utawala wa Khedive Ismail. Alitengeneza mdomo wake kutoka “Bulaq Misr” huko Kairo na mwisho wake katika Bahari ya Shamu, huko mji wa Suez, basi Maji ya Mto Nile yalitiririka huko mnamo majira ya joto na majira ya baridi. Kwa kufanya hivyo, eneo lenye rutuba limebadilishwa na sehemu kubwa ya eneo lake limefufuliwa. Huko, tulipata bustani safi kabisa, ngano, shayiri, alfalfa, na aina nyingi za mboga zilipandwa kando ya mfereji.”

Na Ufaransa ilipofanikiwa kuchimba mfereji mnamo Aprili 25, 1859 , na iwe njia  inayounganisha Bahari ya Shamu na Bahari ya Mediterania na ilifunguliwa kwa urambazaji mnamo  Novemba 17, 1869 , na mji wa Suez ukawa na umuhimu wa kimataifa kama jiji la daraja la kwanza kibiashara, kitalii na kiviwanda, Ufaransa haikupata jina ambalo Ulimwengu wangu unauita isipokuwa Suez; Kama ilivyojulikana kama “Mfereji mdogo wa Suez” au Mfereji wa Suez, kwa sababu ya umaarufu wa kimataifa wa Suez, miji yote kwenye mfereji huo ni miji ya kisasa iliyozaliwa mnamo karne ya 19, isipokuwa Suez, ambayo ina historia ndefu ya biashara ya kimataifa.

Pamoja na kuanzishwa kwa Mfereji wa Suez, ujali mkubwa ulitolewa kwa miji mipya: PortSaid, Ismailia na PortFouad, kwa bahati mbaya, Suez ilianza kupoteza umuhimu wake kidogo kidogo, haswa kwa mkusanyiko wa makazi ya wageni kati ya wafanyikazi wa Mfereji huo katika miji mipya hii.

Ila Suez haukupoteza umaarufu wake wa kimataifa.Wakati uchokozi wa pande tatu ulipotokea – au vita vya 1956 – tunakuta nchi za Magharibi zikiita “Vita ya Suez”, ingawa vita hivyo vilikuwa mbali na mji wa Suez, kama ilivyopiganwa huko. haswa katika PortSaid, lakini huu ni uchawi na nguvu ya historia.

Suez ulijitahidi dhidi ya uvamizi wa Waingereza na wanawe waliandika hadithi za ajabu za kishujaa kwa damu yao safi, kama vita vya wapiganaji viliundwa kutoka kwa wana wa jiji ambao walikuwa wakishambulia kambi za Uingereza nje ya jiji na walipigana vita vikali dhidi ya adui. kwenye ardhi yake, na wakati Rais Gamal Abdel Nasser alipotangaza uamuzi wake wa kihistoria wa kutaifisha Mfereji wa Suez mwaka 1956, Suez ulikabiliwa na uchokozi wa pande tatu uliofanywa na Uingereza, Ufaransa na Israel, na mashujaa wa upinzani maarufu huko PortSaid, Ismailia na Suez waliweza kusimama imara.

 Kufuatia kushindwa kwa Juni 5, 1967, vita vya upinzani viliundwa hivi karibuni, na mnamo Julai 14,15, 1967  Adui alijaribu kutua baadhi ya chembe chenye mfereji huo kwa lengo la kukalia nusu ndefu  ya mfereji huo sambamba na bara la mashariki mwa mfereji huo na kuinua bendera ya Israel juu ya shamandora  iliyowekwa kwenye mfereji unaofafanua njia ya urambazaji, na mara tu meli hizo zimekaribia Shamandora na mashujaa wakiongozwa na Shujaa mkubwa Mohammed Abd Rabu, afisa mmoja wa Mfereji huo, waliweza kuwakamata maafisa na wanajeshi wa Israel, na walikuwa mateka wa kwanza kukabidhiwa kwa jeshi.Baada ya operesheni hii na kushindwa kwa uchokozi kufikia malengo yake, ilishambulia nyumba, misikiti na makanisa kwa makombora mazito ya risasi. kutoka mashariki mwa mfereji ili kudhoofisha ari na kuondoa upinzani maarufu. Viwanda vya mafuta havikuepushwa na ndege za adui zilizokuwa zikiwanyeshea kwa makombora, hivyo uamuzi ukatolewa kwamba ilikuwa ni lazima kupunguza msongamano wa watu wa jiji hilo ili kutoa nafasi kwa majeshi kukabiliana na adui. Kamati ya Usalama wa Taifa iliamua Agosti 8, 1967 , mbele ya magavana wa miji mitatu ya Mfereji, kuondoa idadi ya watu na kuweka idadi ya chini ya wafanyakazi na wafanyakazi.Serikali na sekta ya umma, na jiji hilo lilikuwa tupu. idadi ya watu, kwani serikali iliwapatia makazi yanayofaa katika miji mingi ya Jamhuri.

Na mnamo mapigano ya Vita vya Oktoba mwaka 1973, Israel ilijaribu kurudisha ukuu wake Duniani  na kushinda majeshi ya Misri waliovuka mfereji huu, ambapo katikati ya usiku wa Oktoba 1973, Majenerali wawili wa Israel walifikia mwanzo wa mji wa Suez wakati vikosi vya Jeneral Magen wanapojaribu kutenga Suez kutoka mji mkuu, ingawa vikosi vya Israel vilipoteza takribani vifaru 200 wakati wa kusonga mbele, ila mwishoni mwa usiku wa Oktoba 23  ilikuwa katika mwanzo wa Suez iliyokuwa na lengo ili kuhakikisha moja ya vita vikubwa vya kutetea ardhi na heshima na ifanye kutoka mwanzo wake makaburi ya wavamizi.

Na katika mwanzo wa  siku ya Oktoba 23, Raia wa Suez waligundua kwamba vikosi vya Israel vilikuwa karibu kushmbulia mji huu kwa hiyo, kila mmoja katika mji huu alijitayarisha kuandaa ardhi, na kwa mujibu wa kutopatikana vikosi vyovyote vya kijeshi vya kawaida huko Suez wakati huo, basi wananchi walitegemea silaha nyepesi na ulinzi ukawa ni jukumu la Polisi na viongozi wa Jumuiya ya Sinai ya Kiarabu,  iliyojumuisha vikundi vya mashujaa bora zaidi, na mnamo siku yenyewe Baraza la Usalama lilitoa uamuzi wa pili ambao ni Usitishaji wa mapigano na kuanza utumie kuanzia saa moja asubuhi ya siku ya Oktoba 24,1973.

Pamoja na mwanzo wa siku ya Oktoba 24 adui alianza kubomoa mji kwa mashambulizi ya anga, kisha silaha zilishiriki katika ulipuaji wakati mashujaa walianza kujiandaa na waligundua kwamba ulipuaji unaepuka mlango wa mji, kwa hivyo waligundua kwamba adui watatumia mwanzo huo ili kuvamia mji huo, na kwa haraka maeneo ya kuvizia yalirekebeshwa, na kama walivyodhani vifaru vya Israel vilianaza kusonga mbele kwa shoka tatu :

Mhimili wa pembetatu : Ni Lango la magharibi la mji huko barabara kuu inayotoka Kairo kuelekea Suez na upanuzi wake ni barabara ya jeshi na mtaa wa Al-Arbaeen.

Mhimili wa Al-Janini : kupitia barabara yaliyotoka Ismailia ambapo mlango wa Kaskazini wa Suez hadi eneo la Al-Huwais halafu barabara ya Sedki na kuelekea mtaa wa Al-Arbaeen.

Mhimili wa Al-zaitiya : Ni mlango wa Kusini wa Suez kutoka upande wa bandari ya Al-Adabia na Ataqa kando ya pwani na kusambaza hadi jengo la mji wa Suez na barabara iliyoelekea Bort Tawfik.

Mashujaa waliandaa mashambulizi ya kuvizia kwenye mihimili mitatu hiyo basi, kuna shambulio kuu na shambulio dogo kadhaa kwenye daraja la Al-Huwais kando ya mhimili wa pembetatu na shambulio kuu katika slaidi za Al-Baragel katika barabara ya jeshi na lenye baadhi ya wanajeshi na Polisi na raia kwa uongozi wa Ahmed Abo Hashem na Fayez Hafez Amin kutoka Jumuiya ya Sinai ya Kiarabu, na kwenye mtaa wa Al-Arbaeen kuna shambulio lingine linajumuisha Mahmoud Awad Kiongozi wa mashujaa pamoja na Mahmoud Taha na Ali Siyak wakiwa ni wananchi pamoja na baadhi ya wanajeshi na Polisi, na shambulio lingine katika barabara ya reli kando ya makaburi ya mashahidi na linajumuisha Mahmoud Sarhan na Ahmed Atefi na Ibrahim Youssef pamoja na baadhi ya wanajeshi na Polisi, na shambulio lingine linazungukia mtaa wa Al-Arbaeen linajumuisha Abdulmoneim Khaled na Ghareb Mahmoud kutoka Jumuiya ya Sinai pamoja na wengine, shambulio lingine katika jengo la mji liliongozwa na Luteni Hassan Osama Al-Asr pamoja na wanajeshi wengine.

Suez ikawa ikizungukwa na vikosi viwili vya silaha, na kabla ya alfajiri wakati usitishaji wa mapigano ulitekelezwe, vikosi vya adui vilianaza kusonga mbele na viliingia mji huo bila upinzani, na mpango wa mashujaa ulikuwa ni kuingia vikosi vya Israel kwenye mtego kisha kuvizungukwa na huo ni  mpango wenyewe wa wananchi wa mji wa Rasheed wa Kimisri waliutumia dhidi ya kampeni ya Frazier ya kiingereza mwaka 1807, na vifaru vya Israel vilianaza kutembea kama utembeleaji ndani ya mji uliyoonekana tupu, hata baadhi ya wanajeshi wa Israel walichukua kumbukumbu barabarani.

Ghafla, Suez ulifungua milango ya moto mbele ya uchokozi wa Israeli, na vita vikali vikatokea kati ya mashujaa na vikosi vya adui, na makabiliano makali zaidi yalifanyika katika uwanja wa Arbaeen, ambapo Mahmoud Awad na kundi lake walikabiliana na safu ya jeshi la mizinga, na Awad alifyatua makombora matatu ya RBJ ambayo hayakuwa na ufanisi, na shambulio hilo lililokuwa kwenye Jumba la Sinema la Kifalme, likahamia kumuunga mkono Mahmoud Awad na wakati ambapo tanki kubwa la Centurion lilikuwa likisonga mbele, shujaa Ibrahim Suleiman alitayarisha silaha yake na kurusha risasi moja kwa moja kupenya kwenye mnara wa tanki na kuangusha kichwa cha kamanda wake, ambaye maiti yake ilianguka ndani ya tanki, hivi kwamba wafanyakazi wake walipiga mayowe ya kutisha na kukimbia kwa hofu, nyuma yao wafanyakazi wa mizinga yote nyuma yake.

Wapiganaji wa msituni waliwafyatulia risasi askari wa adui kutoka kila inchi katika uwanja wa Arbaeen, hivyo waliogopa na kuingiwa na hofu, wakaondoka kwenye vifaru kutafuta mfuniko wowote, wakakuta kituo cha polisi cha Arbaeen tu mbele yao. shahidi wa kwanza wa Suez alianguka, shujaa Ahmed Abu Hashem, kaka yake shahidi Mustafa Abu Hashem, ambaye aliuawa shahidi mnamo Februari 8, 1970.

Baada ya kuharibiwa kwa magari mengi ya kivita ya Israel yaliyoingia mjini, vita vilijikita kwenye jengo la kituo cha polisi cha Arbaeen baada ya askari wa adui kukimbilia humo, na waviziaji wote walihamia kukizingira kituo hicho na kufyatua risasi kutoka pande zote. Ibrahim Suleiman, bingwa wa mazoezi ya viungo, akiwa na Ashraf Abdel Dayem, Fayez Hafez Amin, na Ibrahim Youssef, na mpango huo uliandaliwa ili Ibrahim Suleiman atumie uwezo wake na utimamu wake wa kimwili kuruka ukuta wa sehemu hiyo, lakini risasi ya hila kutoka adui alimwangusha kama shahidi juu ya ukuta wa sehemu hiyo, na mwili wake ukabaki ukining’inia kwa siku nzima hadi fedayeen walipoweza kumponya chini ya shambulio hilo kali.

Jaribio la pili lilitoka kwa mashujaa Ashraf Abdel Dayem na Fayez Hafez Amin, ambao waliamua kuvamia sehemu hiyo kutoka mbele, na baada ya kusogea chini ya kifuniko cha moto, chaneli ya adui iliwafyatulia risasi, hivi kwamba Ashraf akaanguka kama shahidi. kwenye ngazi ya sehemu, na mwenzake Fayez alianguka kama shahidi karibu na mtaro ndani ya sehemu hiyo.

Kufikia usiku wa Oktoba 24, 1973 , vikosi vya adui vilikuwa vimeondoka kabisa kutoka kwa Suez baada ya kuacha  vifo na magari yao  ya kivita yakiwa yamesalia, isipokuwa yale yaliyokuwa yamenaswa katika sehemu hiyo.

Suez ulipata ushindi mkubwa na kuwa makaburi ya Wayahudi, na tangu tarehe hii, mji wa Suez husherehekea mnamo Oktoba 24 ya kila mwaka sikukuu yake ya kitaifa, kulingana na uamuzi wa Rais Muhammad Anwar Sadat, ambaye alisema: ( Suez, tarehe ishirini na nne ya Oktoba 1973 , haukuwa ukijilinda, bali ulikuwa ukiitetea Misri yote.

Katika kumbukumbu za Luteni Jenerali Saad al-Din Al-Shazly, Mkuu wa Majeshi ya Misri mnamo Oktoba 1973, alisema: Adui katika jaribio lake la kukalia Suez walipoteza vifo 100  na karibu 500 kujeruhiwa, ingawa walitumia kitengo cha silaha cha brigedi tatu za  kivita na brigedi ya parachuti, shambulio lake lilirudishwa nyuma na wakazi wa Suez na kundi la wanajeshi. Hadithi ya Suez ni ushuhuda mwingine kwa raia wa Misri na uwezo wake wa kuvumilia na kupinga wakati wa shida.

Meja Jenerali Mohamed Abdel Ghani Al-Jamsi, Mkuu wa kamati ya operesheni ya vikosi vya jeshi wakati wa vita vya Oktoba 73, alisema: Vikosi vya Israeli vilishindwa katika mwelekeo wa mji wa Suez mbele ya upinzani maarufu kwa kushirikiana na jeshi dogo  walilokuwa.

Pia tunathibitisha kwa Historia kwamba mnamo Oktoba 26, 1973, sambamba na siku ya kwanza ya Shawwal, siku ya kwanza ya Eid al-Fitr, na wakati Wamisri kote nchini walikuwa wakisherehekea siku ya kwanza ya Eid al-Fitr, Suez ilianza siku ya kwanza ya mzingiro uliodumu kwa siku 101.

Rais Mohamed Anwar Sadat alijua kwamba ikiwa Suez itajisalimisha na kupandisha bendera yake nyeupe kwa vikosi vya Israeli, haitaacha kuandamana magharibi hadi baada ya kuingia Kairo na kuikalia, na Sadat alikuwa na uhakika na ushujaa wa wenye silaha huko Suez.

Suez ilihimili mzingiro wa Israel na Rais Sadat alipopokea ishara ya Meja Jenerali Badawi Al-Khouli, Gavana wa Suez wakati wa mzingiro huo na ombi la jenerali wa Israel alilaani kuukabidhi mji huo, alijua kwamba watu wake hawatasalimika, na Rais Sadat alisema: Endeleeni kupigana. Mwenyezi Mungu yuko nanyi Aliahidi mwenyewe kusali Eid al-Fitr huko Suez kila mwaka baada ya vita na kutimiza ahadi yake mnamo Juni 4, 1974.

 Yote hayo ni muhtasari rahisi wa historia ya Suez adhimu.

Mji huo unajumuisha vitongoji vitano: kitongoji cha Suez: kitongoji cha mjini, ambapo miili mingi ya serikali na maslahi yapo, na kitongoji cha “Arbaeen”: ambacho ni maarufu sana, na kitongoji cha Ataka: na kinajumuisha maeneo mengi ya makazi, viwanda na makampuni, na kitongoji hiki kilitenganishwa kuwa viwili (kitongoji cha Faisal, kitongoji cha Al-Sabah na Ataqa), kitongoji cha Faisal: Kina maeneo ya makazi hadi barabara ya Kairo na kitongoji cha Ataqa, na kitongoji cha Al-Janin: Ni hasa vijijini( Ni hali ya kimashamba).

Una sifa na alama kadhaa za kale na za kisasa zilizoanzia enzi tofauti za kihistoria katika enzi zote, kwa mfano:

Oyoun Musa

Ikihusishwa na Nabii Musa, kilomita 30 kutoka Handaki la Mfiadini Ahmed Hamdi upande wa mashariki huko Sinai, macho ya Musa ni kundi la chemchemi za asili za uwezo tofauti, idadi kubwa ambayo imefutwa, ambayo ni maji safi ya artesia pamoja na kundi la Mitende.

Al Ain  Al Sokhna

Mbwozi wa asili wa chokaa wenye joto la takriban nyuzi 40 iko chini ya mguu wa Mlima Ataqa, na maji yake hutiririka moja kwa moja kwenye maji ya Ghuba, na ni moja ya maeneo mazuri zaidi ya asili ambapo Ghuba ya Suez inakumbatia Mlima Ataka katika kumbatio zuri ambalo ni nadra isipokuwa katika eneo hili, na ni moja ya vivutio vya utalii na mazingira pamoja na uwepo wa baadhi ya miamba ya matumbawe katika eneo hilo, ambayo ni furaha kwa wapenda mbizi.

Makaburi ya Geneva

Moja ya maeneo muhimu ya akiolojia kama ilivyo kituo cha Kifarao cha Szostris (nasaba ya 12) inayotoka katika Maziwa Madogo hadi Geneva, na kuna nyufa nyingi za ufinyanzi katika eneo hilo,  nyingi zilizoanzia vipindi vya Ptolemaic na Kirumi, pamoja na baadhi ya makaburi ya usanifu na tanuru zilizotumika kuyeyusha vyuma na sekta ya Gilasi.

Makumbusho ya Kitaifa

Ina mabaki 1,228  wakati mmoja yaliyotazamwa yanasimulia hadithi ya mji wenye historia. Historia ya Suez imesimuliwa katika zama za Kifaransa, Kirumi na Kigiriki na enzi za ukosefu wa ajira hadi ilipofikia enzi za Kiislamu, na jinsi Suez daima amekuwa shupavu katika zama hizi na lango la mashariki la Misri limeloendelea kuwa imara katika enzi na daima imara.

Handaki la  Shahidi Ahmed Hamdi

Handaki hilo lilipewa jina la Meja Jenerali Mhandisi / Ahmed Hamdi, mmoja wa mashujaa wa Oktoba katika Kikosi cha Wahandisi, aliyeuawa kishahidi katika eneo moja la handaki, na handaki linaanzia barabara ya mkataba (Suez / Ismailia) hadi barabara inayounganisha na Ras Sidr na Abu Rudeis, pamoja na mji wa Qantara Mashariki wenye urefu wa mita 5912, na urefu wa mlango wa magharibi wa handaki ni m 2288, na urefu wa mlango wa mashariki wa handaki ni m 1984.

Mnamo Septemba mwaka jana, handaki la Martyr Ahmed Hamdi “2” lilizinduliwa kwa urefu wa mita 4250, sehemu ya handaki 3250 m, na sehemu ya kina zaidi ya handaki mita 70 kutoka kiwango cha ardhi ya asili, kama mishipa mpya ya maendeleo inayofanikisha uharibifu wa trafiki, huwezesha mwendo wa watu na bidhaa, humaliza mateso ya kusubiri, na hufanya kazi ili kupunguza shinikizo kwenye handaki la zamani na kuchangia kupunguza muda wa usafiri, pamoja na kuunganisha Sinai na bonde na delta.

Al-Nuqtat Al-Hasina

Ni moja ya pointi za mstari wa Bar Lev, ambao Israeli iliujenga kando ya mfereji wa Suez, wakidhani kwamba askari wa Misri hawezi kuupenya, na ulijengwa juu ya kilele cha juu, ukitazama Ghuba ya Suez, na jeshi la Israeli liliipatia vifaa kutoka reli  na silaha zake zilizunguka kwenye mhimili wa umeme na milango yake ilikuwa chuma safi kilichofungwa moja kwa moja.

Chuo Kikuu cha Suez

Taasisi ya elimu ya kisayansi ndani ya kundi la vyuo vikuu vya umma na vya kibinafsi vya Misri. Ilianzishwa kwa kujitenga na Chuo Kikuu cha Mfereji wa Suez kwa mujibu wa Agizo la Rais Na. 193 ya tarehe 22 Agosti 2012.

Kinajumuisha vitivo zaidi ya 12 kwa lengo la kutoa mazingira ya elimu ambayo yana uwezo wa kufundisha, kujifunza na kuendana na kasi ya maendeleo ya teknolojia, na changamoto za jamii kwa wahitimu na utafiti wa kisayansi, ili kuendeleza jamii ya Misri na ushiriki wa vyuo vikuu Duniani katika kukidhi  mahitaji ya binadamu. Na kushiriki katika kujenga ustaarabu wa hali ya juu kama kizuizi cha maendeleo ya binadamu.

Kisiwa cha kijani

Kisiwa cha kijani kiko katikati ya Ghuba ya Suez, ili iwe mbali na kila moja (Lango la kuingilia mfereji kilomita 3, Bandari ya Suez, Bandari ya Adabiya, Shatt 2 km, Ras Sidr, Bandari ya Sokhna 4 na 5 km).

Kilikuwa ndani ya kambi za Uingereza nchini Misri kabla ya ukombozi, eneo lenye kinga dhidi ya mabomu ya atomiki na lilikuwa kilele cha usumbufu kwa Israeli na eneo la onyo la mapema dhidi ya uvamizi, ingawa eneo lake ni mita 190 * mita 90 tu, lakini lilikuwa na silaha za ardhini, bunduki za kupambana na ndege, hatua ya hali ya hewa na onyo la mapema, Israeli ilifanya kwa nguvu zake zote kampeni dhidi yake kuikalia mnamo 69, na licha ya ubora wa anga, ushujaa na kujitolea kwa jeshi letu kuliwarudisha katika vita vilivyofundishwa katika sayansi ya kijeshi Duniani kote kwa jina la vita vya Kisiwa cha kijani.

Pia ni mabaki ya miamba ya matumbawe iliyoenea sana, kutishia meli, na inadhibiti mlango wa kusini wa mfereji wa Suez, na kusababisha wanasayansi kuweka wingi wa saruji juu yake ili kutodhuru meli zinazopita kwenye mfereji, na kugeuka kuwa kisiwa kwenye mlango wa kusini wa mfereji.

Jumba la Muhammad Ali


Jumba hilo lilijengwa na Muhammad Ali Pasha, ili liwe makao makuu yake wakati wa maandalizi ya jeshi la Misri kwa ajili ya kampeni dhidi ya dola ya Wahhabi katika Rasi ya Uarabuni kwa kufuata amri ya Khalifa wa Ottoman, na ndani ya ukumbi ulio chini ya kuba ya ikulu hii, Muhammad Ali na wanawe Toson na Ibrahim walikutana kusimamia vita dhidi ya Wahhabism katika Hijaz hadi 1818.

Lina ghorofa mbili, sehemu ya mashariki ambayo imezingirwa na kuba ya mbao. Katika pwani tofauti ya jumba hili, Muhammad Ali Pasha mwenyewe alisimama kufuata ujenzi wa meli za kwanza za meli za Misri.

Taasisi ya Sayansi za Bahari

Ni taasisi inayohusiana na Chuo cha Utafiti wa Kisayansi na ina kundi la maabara za kujifunza viumbe mbalimbali vya majini vya samaki, mimea ya baharini, na viumbe vya baharini vinavyoishi katika mikoa ya Bahari ya Shamu, iliyounganishwa nayo ni Makumbusho ya tangisamaki inayojumuisha samaki wengi, na viumbe wengine wa baharini.

Suez imekuwa na bado ni lengo la umakini wa Dunia na kila adui wa Misri daima inaiweka kama shabaha katika vituko vyake kama lango la Misri kupitia Bahari ya Shamu na maji ya Ghuba kwani inafurahia eneo la kimkakati la kimataifa na ina umuhimu wa baharini kama mlango wa kusini wa mfereji wa Suez kwani ndio utawala wa karibu zaidi kwa mji mkuu.

Msikiti wa Abdullah Al Gharib

Ni moja ya misikiti maarufu katika mji huo na mmiliki wake anachukuliwa kama shujaa wa mashujaa wa epics za Kiislamu, ambao walipigana na Waqarmatia,  waliojaribu kudhibiti njia ya Haji, naye ni Mmorocco, na anaitwa Abu Yusuf Aqoub bin Muhammad bin Yaqoub bin Imad na alijulikana kama Mgeni kwani aliuawa mbali na nchi yake na jina lake halikujulikana hadi baada ya kaburi lake kufunuliwa mnamo 1964.

Kuna misikiti mingine, ikiwa ni pamoja na (Arbaeen – Abboud – Abu Alif – Faraj – Shuhada – Badr – Sunnah ya Mtume – Hamza).

Monasteri ya Anba Paula na Monasteri ya Anba Antonios

Kuna makanisa mjini, ikiwa ni pamoja na (Kanisa la Kiinjili – Kilatini – Saint Jesus’Mother- Mtakatifu Anthony na Kiitaliano – Mchungaji Mwema).

Kanisa Katoliki la Kirumi, lililoanzia wakati wa Kaisari Justinian katika karne ya tano na kisha kurejeshwa katika zama zifuatazo, kwa sasa linaitwa Konventi ya Watawa, iliyoko katika eneo la mgeni, na imetembelewa na baadhi ya watu mashuhuri kama vile Napoleon na Ufalme wa Eugenie.

Kuhusu Monasteri ya Mt. Paula na Monasteri ya Mt. Anthony, ni monasteri mbili kongwe za Kikristo katika Jangwa la Mashariki, monasteri ya pili iko takriban kilomita 130 kutoka mji wa Suez halafu kilomita 55 upande wa magharibi, na iko karibu na mji wa Suez kutoka Mkoa wa Bahari ya Shamu, wakati monasteri nyingine iko umbali wa kilomita 155 kutoka mji huo na kisha kilomita 37 upande wa magharibi.

Matembezi ya Watu wa Suez 

Iko kando ya mita 1300, katika eneo la Port Tawfiq katika wilaya ya Suez.

Uwanja wa Suez

Uwanja wa Suez unaweza kuchukua watazamaji 20,500, kituo cha habari kinachoweza kuchukua waandishi wa habari 100 na wataalamu wa vyombo vya habari, pamoja na kuzuka kwao, intaneti ya kasi, vifaa vya mtandao wa eneo pana, na vifaa vya kupokezana vya Wi-Fi, kulingana na kebo ya nyuzi ya kasi kwa uwanja. Baadhi ya mechi zilichezwa katika Kombe la Dunia la Vijana mwaka 2009.

Check Also
Close
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"