Habari

Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Katibu wa Baraza la Usalama la Kitaifa la Shirikisho la Urusi

Ali Mahmoud

0:00

Balozi Ahmed Abu Zeid, Msemaji rasmi wa Wizara ya Mambo ya Nje, alisema kuwa Bwana Sameh Shoukry mnamo Jumanne 31 Januari hii, alikutana na bwana “Nikolai Patrushev”, Katibu wa Baraza la Usalama la Kitaifa la Shirikisho la Urusi wakati wa ziara yake ya kisasa kwa Moscow.

Kuhusu mada muhimu zaidi zilizoshughulikiwa wakati wa mkutano huo, Msemaji rasmi huyo alieleza kuwa mashauriano yalishughulikia masuala maarufu zaidi ya mahusiano ya nchi hizo mbili kati ya Misri na Urusi na njia za kuyaendesha mbele kwa njia inayofikia maslahi ya nchi hizo mbili, ambapo historia ya mahusiano ya Urusi na Misri ilisifiwa kama msingi imara kwa kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mikubwa nchini Misri, wa maarufu zaidi ni Kituo cha Dabaa cha Nishati ya Nyuklia na Ukanda wa Viwanda wa Urusi kwenye Eneo la Kiuchumi la Mfereji wa Suez kama vituo vyema vilivyongezwa kwa historia ya mahusiano kati ya nchi hizo mbili.

Katika muktadha huu, pande za Misri na Urusi zilikuwa na uangalifu wa kuonesha nia ya kusherehekea Agosti ijayo maadhimisho ya miaka 80 ya kuanzishwa kwa mahusiano ya kidiplomasia kati ya Misri Na Urusi.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje aliongeza kuwa Bw. Sameh Shoukry alisikiliza maelezo marefu kutoka kwa Afisa wa Urusi kuhusu maendeleo ya mzozo wa Urusi na Ukraine, ambapo alisisitiza umuhimu wa kuweka suluhisho la kisiasa kumaliza mzozo huo, ambapo una athari kubwa kimataifa na kikanda, kwa njia ambayo inaathiri nchi zinazoendelea, miongoni mwake Misri. walikubaliana juu ya umuhimu wa kuendelea na mashauriano kupitia njia mbalimbali za nchi mbili ili kubadilishana maoni juu ya masuala ya kikanda na kimataifa yenye maslahi ya pamoja.

Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"