Siasa

WAZIRI MKUU AAGIZA RCs, DCs, VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAHIMIZE KILIMO CHA CHIKICHI

Ahmed Hassan

0:00

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na viongozi wa vyama vya siasa watumie majukwaa waliyonayo kuhimiza kilimo cha michikichi ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo nchini.
“Viongozi wote wa Mikoa, Wilaya, na wa vyama vya siasa mnayo majukwaa ya kukutana na wananchi kila wakati. Twendeni tukahamasishe wananchi walime michikichi kwa sababu ni zao litakalowapatia fedha kwa muda mrefu,” amesema.
Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Februari 26, 2023) wakati akizungumza na wadau wa zao la chikichi mkoani Kigoma kwenye ukumbi wa NSSF. Wadau hao wanajumuisha wakulima, wazalishaji miche, wakamuaji mawese, viongozi wa vijiji, viongozi wa taasisi za fedha, viongozi wa wilaya, Halmashauri na mkoa.
Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"