Makala za maoni

Kiswahili kwa kufikia Amani na Ustawi

Mervat Sakr

0:00

Kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazotumika sana katika familia za lugha za Kiafrika, tena ni maarufu zaidi Barani Afrika, na kati ya lugha kumi zinazozungumzwa sana Duniani, basi kuna wasemaji wa Kiswahili zaidi ya milioni 200, hivyo Umoja wa Mataifa uliamua kuainisha Julai 7 ya kila mwaka kusherehekea Siku ya Kiswahili Duniani ili kukuza matumizi yake kwa Umoja na Amani, tena kukuza utofauti wa kiutamaduni, kujenga uelewa na kukuza mazungumzo kati ya ustaarabu inayokuza Umoja katika utofauti, uelewa wa kimataifa, uvumilivu na mazungumzo.

Kiswahili ni mchanganyiko wa vipengele vya lugha vinavyotokana na lugha ya Kiarabu na kutoka  lugha zinazotumika Barani Afrika na bara la Ulaya, pia nchi ambazo lugha ya Kiswahili ni lugha ya kitaifa au rasmi ni Tanzania, Kenya, na pia ni lugha ya kawaida miongoni mwa watu wa Uganda, Burundi, Rwanda, kaskazini mwa Msumbiji na kusini mwa Somalia, pamoja na uwepo wake miongoni mwa watu wa Malawi, Zambia, Sudan Kusini na nchi nyingine.

Ilitajwa katika tovuti rasmi ya UNESCO kuwa Kiswahili inafundishwa katika baadhi ya Vyuo Vikuu na Vitivo vikubwa Duniani kote, na Umoja wa Mataifa ulianzisha kitengo cha lugha ya Kiswahili katika Redio ya Umoja wa Mataifa, hadi ikawa lugha pekee ya Kiafrika ndani ya Umoja wa Mataifa, na pia ukataja kuwa kwa karne nyingi lugha ya Kibantu imeibuka kama aina ya mawasiliano ya kawaida katika sehemu nyingi za Afrika, na pamoja na yote hapo juu, lugha ya Kiswahili imepitishwa kati ya lugha zilizopitishwa katika Umoja wa Afrika.

Tena ni muhimu sana kuashiria kusherehekea Umoja wa Mataifa kwa Siku ya Kiswahili Duniani pamoja na kauli mbiu ya Kiswahili kwa Amani na Ustawi, basi kuna wasemaji wa Kiswahili zaidi ya milioni 200, endapo ni moja ya lugha za Kiafrika zinazozungumzwa sana, zikiwa na lahaja kuu zaidi ya 15.

Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"