Habari

Rais El-Sisi akutana na Rais Putin

Zeinab Makaty

0:00

Rais Abdel Fattah El-Sisi alikutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin, Jumatano Julai 7, katika “Kasri la Constantine” huko mjini Petersburg.

Ahmed Fahmy, msemaji rasmi wa Ofisi ya Rais wa Jamhuri, alisema kuwa Rais wa Urusi alikaribisha ziara ya Rais nchini Urusi, na akisifu jukumu muhimu la Rais katika kuzindua toleo la kwanza la Mkutano wa kilele wa Urusi na Afrika wakati wa urais wa Misri wa Umoja wa Afrika 2019, uliolenga kuunga mkono na kuimarisha mahusiano ya kipekee na ya kihistoria kati ya bara la Afrika na Urusi, pamoja na kuimarisha mashauriano kati ya pande hizo mbili kuhusu jinsi ya kutatua changamoto za pamoja.

Pia, Rais Putin aliashiria umuhimu anaotilia kuendelea uratibu na mashauriano na Mheshimiwa Rais kuhusu masuala mbalimbali ya kikanda na kimataifa yenye maslahi kwa pamoja, na kuthamini kwake jukumu la Misri kama nguzo muhimu ya usalama na utulivu katika Mashariki ya Kati na Afrika.

Msemaji huyo aliongeza kuwa Rais alielezea nia yake ya kuimarisha mahusiano ya ushirikiano na Shirikisho la Urusi ndani ya muktadha wa maendeleo endelevu yaliyoshuhudiwa na mahusiano hayo, yaliyofikia mwisho wa kusaini Mkataba wa Ushirikiano wa Mkakati wa kina katika 2018, na akisifu katika suala hili ushirikiano uliopo wa nchi mbili katika nyanja nyingi na miradi ya pamoja inayoendelea, hasa mradi wa kuanzisha eneo la viwanda la Urusi katika Eneo la Uchumi wa Mfereji wa Suez, na mradi wa kuanzisha kiwanda cha nyuklia cha Dabaa.

Mheshimiwa Rais pia alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi ili kuendeleza matokeo halisi na ya vitendo kutoka kwa mkutano wa Urusi na Afrika kwa manufaa ya watu wa Afrika kwanza, kwa kuzingatia kuwa mkutano huo una lengo la kuanzisha ushirikiano endelevu kati ya Urusi na nchi za Afrika, akielezea katika suala hili utayari wa Misri kuimarisha nyanja mbalimbali za ushirikiano wa pande tatu kati ya nchi hizo mbili Barani Afrika.

Msemaji huyo alisema kuwa marais hao wawili , wakati wa mkutano huo walijadiliana maendeleo ya masuala kadhaa yanayohusiana na uhusiano wa nchi mbili, ikiwa ni pamoja na kiwanda cha nyuklia cha Dabaa na miradi ya eneo la viwanda la Urusi, pamoja na ushirikiano katika uwanja wa kuendeleza muktadha wa usafiri na reli, pamoja na kiwango cha ushirikiano wa pamoja katika uwanja wa usalama na kupambana na ugaidi.

Kwa upande mwingine, marais hao wawili walipitia masuala ya kikanda na kimataifa ya maslahi ya pamoja na kubadilishana maoni juu ya migogoro kadhaa katika Mashariki ya Kati, ambayo kimsingi ni maendeleo ya Sudan, Syria na Libya, na suala la Palestina, ambapo maono yalikubaliana kuendeleza juhudi za kurejesha na kuimarisha usalama, utulivu na amani kwa nchi za kanda, kwa njia inayohifadhi umoja na uhuru wa maeneo yao na haki halali za watu wao.

Rais Putin pia alimfahamisha Rais maendeleo ya mgogoro wa Urusi na Ukraine, ambapo Rais alithibitisha msaada wa Misri kwa juhudi zote ambazo zitaharakisha suluhisho la kisiasa la amani la mgogoro huo ili kupunguza mateso ya binadamu yaliyopo, kumaliza athari mbaya za kiuchumi kwa nchi za ulimwengu, hasa nchi zinazoendelea na za Afrika, na kudumisha usalama wa kimataifa na utulivu.

Back to top button