Habari

Rais El-Sisi afanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Armenia “Nikol Pashinyan”

Mervet Sakr

0:00

Msemaji wa Urais wa Misri alisema kuwa Bw. Pashinyan alielezea furaha yake na ziara ya Rais nchini Armenia kwa mara ya kwanza, akisisitiza nia ya nchi yake katika kuendeleza mahusiano yake na Misri kwa kuzingatia umuhimu wa jukumu lake katika Mashariki ya Kati na Afrika, pamoja na sera yake ya kigeni huru na yenye usawa katika kukabiliana na changamoto ngumu katika mazingira yake ya kikanda yenye misukosuko.

Waziri Mkuu wa Armenia pia alipongeza mahusiano maalum ya kihistoria na ambao kwa muda mrefu umezifunga nchi hizo mbili rafiki, na kasi iliyoshuhudiwa na mahusiano hayo katika kipindi cha hivi karibuni kupitia kubadilishana ziara za kiwango cha juu, ambayo ya hivi karibuni iliyokuwa ushiriki wa Rais wa Armenia katika Mkutano wa Hali ya Hewa Duniani COP27 uliofanyika Sharm El-Sheikh Novemba mwaka jana.

Msemaji rasmi alisema kuwa Mheshimiwa Rais alimshukuru Waziri Mkuu wa Armenia kwa mapokezi mazuri, akielezea furaha yake ya kutembelea Armenia na nia ya kuimarisha na kuendeleza mahusiano kati ya nchi hizo mbili rafiki katika nyanja mbalimbali, haswa kwa kuzingatia mahusiano imara na yaliyopanuliwa kati ya nchi hizo mbili, akisifu nafasi nzuri na za kuthaminiwa za Armenia kuelekea Misri, na maendeleo makubwa yaliyopatikana katika mahusiano kati ya nchi hizo mbili katika kipindi cha mwisho kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili kushinikiza mahusiano ya pande mbili kwa upeo mpana.

Wakati wa mazungumzo hayo, Rais pia alikagua mapya ya mpango wa maendeleo uliopitishwa na serikali, na miradi ya kitaifa inayotekelezwa kwa fursa za uwekezaji wanazotoa, akisisitiza nia yake ya kufikia hatua ya ubora katika eneo la ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, haswa kwa kuhimiza ushirikiano kati ya jumuiya ya wafanyabiashara katika nchi hizo mbili kwa njia inayoonekana katika maendeleo ya kiasi cha kubadilishana biashara na uwekezaji, pamoja na kufanya duru ya sita ya Kamati ya Pamoja ya Ushirikiano wa Kiuchumi, Sayansi na Ufundi huko Kairo haraka iwezekanavyo kwa kuzingatia jukumu lake kama utaratibu wa kitaasisi wa mazungumzo. Mbali na kuimarisha ushirikiano wa pamoja katika nyanja kadhaa za kuahidi kama vile nishati, miundombinu, teknolojia ya habari, viwanda vya chakula na dawa, pamoja na kuunga mkono juhudi za Misri za kuanzisha eneo huru la biashara na nchi za Umoja wa Kiuchumi wa Eurasian kwa maslahi ya pamoja ya pande zote mbili, kwani bidhaa za Misri zinafaa mahitaji ya nchi hizo kwa ubora na bei.

Msemaji rasmi huyo aliongeza kuwa mazungumzo hayo pia yalishuhudia kubadilishana maoni juu ya faili na migogoro kadhaa ya kikanda, na tathmini ya athari zake juu ya usalama wa bara la Ulaya, ambapo Waziri Mkuu wa Armenia, kwa upande wake, alithamini juhudi husika za Misri za kufikia suluhisho la kisiasa kwa mizozo mbalimbali mashariki ya kati.

Katika ngazi ya Ulaya Mashariki na Caucasus ya Kusini, pande hizo mbili zilikubaliana juu ya haja ya kuimarisha uratibu na mashauriano juu ya masuala na faili za maslahi ya pamoja katika suala hili, hasa kuhusiana na maendeleo ya mgogoro wa Urusi na Ukraine na athari zake za kiuchumi ulimwenguni.

Rais na Waziri Mkuu Pashinyan pia walikubaliana juu ya haja ya kuimarisha ushirikiano wa pamoja wa kupambana na uhamiaji haramu kupitia mtazamo kamili, na kufanya kazi ili kuondoa sababu kuu zinazohimiza jambo hili, pamoja na kukagua maendeleo ya hivi karibuni katika kupambana na ugaidi, yanayotishia nchi mbalimbali Duniani, ambapo umuhimu wa mshikamano wa jumuiya ya kimataifa kukabiliana na jambo hilo ulisisitizwa.

Back to top button
اكتب رسالتك هنا
1
تواصل معنا
اهلا بك في بوابة " مصر الآن"