Habari

Rais Abdel Fattah El-Sisi aelekeza Uzinduzi wa Mpango wa Ushirikiano na Vyuo Vikuu vya Kimataifa katika Mji Mkuu Mpya wa Utawala ili kudhamini Idadi ya Wanafunzi bora wa Misri ya Juu kusoma katika Vyuo Vikuu hivi vya Kimataifa katika Mji Mkuu

Mervet Sakr

0:00

Jumatatu, Rais Abdel Fattah El-Sisi alikutana na Waziri Mkuu Dkt. Mostafa Madbouly, Waziri wa Nyumba, Huduma na Jamii za Mijini Dkt. Assem El-Gazzar, Mwenyekiti wa Mamlaka ya Masuala ya Fedha ya Jeshi Luteni Jenerali Ahmed El-Shazly, Mshauri wa Mkuu wa Mipango Miji Meja Jenerali Amir Sayed Ahmed, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni mpya ya Mitaji ya Utawala na Mhandisi Khaled Abbas, na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Uhandisi wa Majeshi Meja Jenerali Ahmed Al-Azazi.

Mshauri Ahmed Fahmy, Msemaji Rasmi wa Urais wa Misri, alisema kuwa mkutano huo ulipitia hali ya kiutendaji wa kazi zinazoendelea katika Mji Mkuu Mpya wa Utawala, ikiwa ni pamoja na vifaa, barabara za ndani na shoka, vitongoji vya makazi na maeneo ya biashara, kwa kuzingatia kuanza kwa mabadiliko ya taratibu ya wizara kwenda wilaya ya serikali katika Mji Mkuu wa Utawala.

Mkutano huo pia uligusia juhudi za kuunganisha vishoka na barabara za Mji Mkuu Mpya wa Utawala na vitongoji vyote na sekta za kubwa zaidi Kairo (Greater Cairo), kupitia usafiri wa kisasa wa wingi, pamoja na kuwasilisha mfumo wa usafiri ndani ya mji mkuu wenyewe, na nafasi ya kiutendaji wa kituo Kikuu cha Mabasi.

Rais alielekeza ufuatiliaji makini wa mara kwa mara wa kazi na miradi mbalimbali ya ujenzi katika Makao Makuu ya Utawala, huku akizingatia viwango vya juu vya ubora, usalama na utawala kwa mujibu wa mifumo ya kisasa ya kiteknolojia katika uwanja huo, pamoja na kuzingatia mfumo wa uendeshaji, usimamizi na matengenezo kwa vitongoji na vituo vya mji mkuu, hususan eneo la kati, wilaya ya serikali na vituo mbalimbali vya umma, ili kuhakikisha uendelevu wa viwango vya ubora wa kimataifa vimevyoanzishwa, na kuvitunza kwa kiwango cha juu.

Msemaji Rasmi huyo aliongeza kuwa Rais Abdel Fattah El-Sisi aliagiza kuzinduliwa kwa mpango huo kwa kushirikiana na vyuo vikuu vya kimataifa katika Mji Mkuu Mpya wa Utawala ili kudhamini idadi kubwa ya Misri ya Juu kusoma katika vyuo vikuu hivi vya kimataifa katika mji mkuu, sambamba na sera ya serikali ya kuwaruhusu wananchi wote kutoka sehemu mbalimbali za Jamhuri kunufaika na fursa na huduma bora zinazopatikana katika Mji Mkuu Mpya wa Utawala.

Back to top button