Habari

Misri yalaani mashambulizi ya kigaidi nchini Mali

Mervet Sakr

0:00

Jumamosi, Septemba 9, Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje imelaani vibaya mashambulizi mawili ya kigaidi yaliyotokea kaskazini mashariki mwa Mali, na kusababisha makumi ya watu wahanga na waliojeruhiwa.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imetoa rambirambi za dhati kwa serikali na watu wa Jamhuri ya Mali, na familia za wahanga wa tukio hilo la kigaidi na matakwa yake ya kupona haraka kwa majeruhi.

Katika taarifa yake, Misri imethibitisha kulaani vitendo hivyo vya kigaidi, na kutoa wito kwa Jumuiya ya kimataifa kuungana ili kutokomeza ugaidi kutoka mizizi yake na kukauka vyanzo vyake vya ufadhili na msaada.

Back to top button