Habari Tofauti

Mazungumzo ya Bwawa la Al-Nahda yaanza tena jijini Kairo

Tasneem Muhammad

0:00

Jumapili asubuhi, Agosti 27, 2023, duru mpya ya mazungumzo ya Bwawa la Al-Nahda ilizinduliwa mjini Kairo, kwa ushiriki wa wajumbe wa majadiliano kutoka Misri, Sudan na Ethiopia, kwa kuzingatia taarifa iliyotolewa Julai 13, 2023 na mkutano wa viongozi wa Misri na Ethiopia mjini Kairo pembezoni mwa mkutano wa kilele wa nchi jirani za Sudan, na uratibu na Jamhuri ndugu ya Sudan.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Misri, Dkt. Hani Sweilam, alisisitiza umuhimu wa kufikia makubaliano ya kisheria juu ya sheria za kujaza na kuendesha Bwawa la Al-Nahda, kwa kuzingatia maslahi na wasiwasi wa nchi hizo tatu, akisisitiza umuhimu wa kuacha hatua zozote za upande mmoja katika suala hili, na kwamba kuendelea kujaza na uendeshaji wa bwawa bila makubaliano ni ukiukaji wa Mkataba wa Kanuni uliosainiwa mwaka 2015.

Sweilam amesisitiza kuwa Misri inaendelea kufanya juhudi za juu za kufanya mchakato wa mazungumzo kuwa na mafanikio, akisisitiza imani ya Misri katika kuwepo kwa suluhisho nyingi za kiufundi na kisheria ambazo zinaruhusu kukidhi maslahi ya nchi hizo tatu, na kufikia makubaliano yaliyohitajika.

Back to top button