Habari

Kukabidhi vituo kadhaa vya kila mahali kwa Waziri wa Utafiti wa Sayansi wa Congo kwa kuchangia kupunguza athari za shughuli za Volcano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

0:00

Balozi Hisham Abdel Salam El-Mekoud, Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, alimkabidhi Bw. Gilbert Kabanda, Waziri wa Utafiti wa Sayansi wa Congo, vituo kadhaa vya kila mahali vilivyotolewa kama ruzuku kutoka Taasisi ya Taifa ya Misri ya Utafiti wa Astronomical na Jiofizikia, iliyopangwa kuhamishiwa kwa kituo cha Goma kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ili kusaidia kupunguza athari za uwezekano wa maafa ya shughuli za Volcano katika mkoa huo.

Mhusika huyo wa Congo aliishukuru Misri kwa msaada huo utakaochangia kuwalinda raia wa Congo dhidi ya hatari ya shughuli za Volcano, akisifu mahusiano ya Misri na Congo, yanayoshuhudia maendeleo makubwa mnamo kipindi cha hivi karibuni kwenye nyanja mbalimbali, na kuelezea matarajio yake ya kuendelea kwa ushirikiano huo mnamo kipindi kijacho.

Back to top button