Habari

Dkt. Hani Swailem na Bw. Pal Mai Ding wazindua “Mradi wa Ujenzi wa Visima vya Chini ya Ardhi kwa Matumizi ya Kunywa katika Chuo Kikuu cha John Garing” huko mjini mwa Bor, Jimbo la Jonglei

Ftima Ahmed

0:00

 

Ndani ya mfumo wa ziara yake kwenye nchi ndugu ya Sudan Kusini. Prof. Hani Sweilam, Waziri wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji, na Mheshimiwa Pal Mai Deng, Waziri wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji wa Jamhuri ya Sudan Kusini, walitembelea Jimbo la Jonglei kwenye Nchi ya Sudan Kusini, ambapo walipokelewa na Bw. Mahgoub Bell, Gavana wa Jimbo la Jonglei.

Mawaziri hao walifanya mkutano na Gavana wa Jimbo la Jonglei, aliyekaribisha ziara ya Dkt. Sweilam na ujumbe rasmi ulioambatana naye na Balozi Moataz Mustafa Abdel Qader, Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri nchini Sudan Kusini.

Wakati wa mkutano huo, walijadili msimamo wa miradi imeyokamilika au inatekelezwa na kuwasilisha mahitaji ya upande wa Sudan Kusini wa miradi ya baadaye.

Bw. Mahgoub Bell alipongeza miradi iliyotekelezwa kwa msaada wa Misri, inayohudumia sehemu kubwa ya wananchi na inawakilisha mchango mkubwa katika kuwahudumia wananchi, akiishukuru serikali ya Misri, uongozi wa kisiasa na Dkt. Swailem kwa kutekeleza miradi hiyo.

Baada ya mkutano huo, Mawaziri, Gavana wa Jimbo na Balozi wa Misri nchini Sudan Kusini walikwenda kusherehekea uzinduzi wa “Mradi wa Ujenzi wa Visima vya Chini ya Ardhi kwa Matumizi ya Kunywa katika Chuo Kikuu cha John Garing” huko mjini mwa Bor, Jimbo la Jonglei, kwa hudhuria ya viongozi na maafisa kadhaa kutoka nchi hizo mbili na idadi kubwa ya wananchi katika eneo la mradi.

Katika hotuba yake kwa wasikilizaji. Dkt. Hany Sweilam alielezea furaha yake kwa uzinduzi wa mradi wa visima vya chini ya ardhi katika mji wa Bor, akisisitiza kuwa mradi huu unaakisi dhamira ya Misri ya kuunga mkono juhudi za Nchi ya Sudan Kusini katika kufikia maendeleo endelevu na ustawi kwa wananchi wake, ambayo ndiyo tunayoshuhudia leo chini, ambapo tunasherehekea kwa pamoja uzinduzi wa maji katika kituo cha maji ya kunywa chini ya ardhi, ambayo hubeba mema na maendeleo kwa wananchi na watu katika mkoa huo kwa kuwahudumia karibu watu elfu 4, akieleza kuwa Misri imekamilisha utekelezaji wa vituo 20 vya maji ya kunywa vya chini ya ardhi vilivyo na nishati ya jua katika maeneo ya mbali kutoa maji ya kunywa kwa karibu watu elfu 100, pamoja na utekelezaji wa miradi mingi ya kuvuna maji ya mvua na kupunguza hatari ya mafuriko na kazi za kibali cha magugu ili kuwezesha harakati za urambazaji wa mto na kuchochea harakati za biashara.

Kwa upande wake… Bw. Pal Mai Ding alipongeza jukumu kubwa lililofanywa na Misri katika kusaidia sekta ya rasilimali za maji nchini Sudan Kusini, akiishukuru serikali ya Misri kwa utekelezaji wa mradi huu muhimu, uliochangia kutatua tatizo linalowakabili wanafunzi wa vyuo vikuu kutokana na ukosefu wa maji ya kutosha na safi ya kunywa wakati wa mwaka wa masomo, na kisima hicho pia kitachangia kutoa maji safi ya kunywa kwa wananchi katika maeneo jirani, akitoa wito wa kuendelea msaada wa Misri kwa Sudan Kusini katika uwanja wa maji.

Back to top button